Kutoka Kigongo kwenda Busisi na kurudi kwa kivuko (pantoni) utajionea mandhari nzuri kama hii!
Tuanze safari yetu ya pamoja kutafakari hali na mustakabali wa maisha ya Kijijini Kwetu. Haina maana ya kule nitokako bali hata kwako pia. Yawezekana huna ukakika kama sitafika! Karibu sana
Friday, August 5, 2011
Wednesday, August 3, 2011
Kwenye Utajiri lakini madhila kibao
Hapa ni kwenye kisima cha Lwenge chenye kutoa maji yanayotumika ktk mji wa Geita. Wadosi wanapata maji kutoka kwenye pump inayotoa maji hapo lakini walala hoi wanajipanga foleni kuanzia saa 10 usiku. wengi wao ni akina mama-fikiria hatari zinazowakabili.
Pata taswira ![]()
Maji yametoka Ziwa Victoria kwenda Kahama Shinyanga lakini yaliyoko km 45 tu toka hapa mjini imekuwa kesi! Dah!
Monday, August 1, 2011
Nani wa kutupumzisha?
Wenyeji wanayaita MAGWANGALA…masalia ya mawe toka mgodini (waste rock) yanayouzwa kwa kiroba sh 4000-5000. Kisha huletwa hapa Nyankumbu kwa ajili ya kupondwa, kusagwa na kisha kuoshwa na kupata dhahabu.
Wapondaji ni nani? Wengi ni akina mama na watoto! Ukitaka kujua ama kuona utumikishwaji wa watoto…njoo hapa utajionea.
Pata taswira ![]()
Afya za wanawake, watoto na vijana zi mashakani!
Ukifika pahala hapa na ukasikia kelele za ‘krasha’ hapo utadhani ni boeing inaondoka uwanjani! ![]()