Wakimaliza ndo akili itarudi!!
Tuanze safari yetu ya pamoja kutafakari hali na mustakabali wa maisha ya Kijijini Kwetu. Haina maana ya kule nitokako bali hata kwako pia. Yawezekana huna ukakika kama sitafika! Karibu sana
Thursday, June 30, 2011
Friday, June 24, 2011
Sitashangaa hili likitokea!
Kalonzo na JK (si picha ya Malaysia)
Tarehe 17 June mwaka huu, Makamu wa Rais wa Kenya (Stephen Kalonzo) ametoa kauli ya kushangaza (kwangu).Ndugu Steve Kalonzo alisikika katika eneo la Tiganya wakati wa hafla ya kuchangia fedha shule moja ya upili kuwa ‘ataongea na Rais wa Tanzania, JK, ili Tanzania iruhusu biashara ya MIRAA ama MIRUNGI iruhuhusiwe kuuzwa Tanzania.
Ikumbukwe kuwa mirungi ni zao ambalo liko kwenye kundi la madawa ya kulevya kama bangi ambalo limepigwa marufuku kulimwa na kutumika nchini.
Wiki hii Kalonzo ameonekana na JK kwenye picha wakiwa wanateta walipokuwa nchini Malaysia.
Ndiyo aina ya viongozi tulio nao Afrika wenye kusema ujinga wa aina yoyote na ukakubalika!!!!
kazi ipo!
Sunday, June 19, 2011
Leo Ni Siku yangu ya kuzaliwa!
Friday, June 10, 2011
Weekend Njema!
Tuwemo!
Thursday, June 9, 2011
Ulaji huo!
Kama kweli makosa ya barabarani yatatozwa shilingi elfu hamsini (50,000) basi mimi kama askari wa usalama barabarani naona raha sana kwani utajiri uko bwerere kwangu! Nitabambikiza makosa hata yasokuwepo na hivo kama wewe una makosa matatu ukinipa elfu arobaini (40,000) tu nakuachia. Nikikamata gari lako tu moja kila siku kwa mwezi najihakikishia kuwa na sh 1,200,000/ ambazo ni sawa na mshahara wa katibu wa CCM Taifa!
Aksante Mkulo!
Ngoja niserebuke kidogo!
Friday, June 3, 2011
Walioelimika, Aibu iko wapi?
Watumishi wa umma ambao hawautumikii umma, bali wanajitumikia wao wenyewe
Wanasiasa wanaozungumza, lakini hawasemi lolote
Wapigaji kura ambao wanapiga kura, lakini hawamchagui mtu yeyote
Walimu wanaofundisha ujinga
Mahakimu ambao wanawahukumu watu na wanachukua mlungula
Wanajeshi ambao kila wakati wako katika mapambano na watu ambao inabidi wawalinde
Maaskari ambao hawawezi kuzuia uhalifu kwa sababu wako “busy” na mikakati ya kufanya uhalifu
Watu ambao wanazitumikia pesa
Wacha Mungu ambao badala ya kumhubiri Mungu kwa ajili ya mbingu wanamhubiri Mungu kwa ajili ya tamaa zao
Madaktari ambao badala ya kuokoa maisha, wanayamalizia
Makandarasi ambao wanatengeneza majumba yanayoporomoka na barabara zenye mashimo
Wafanyabiashara wanaouza takataka
Watu wafundishao maadili lakini wao wakiwa hawana maadili
(Credit: Dr Kamanzi, A)
Pata Uhondo toka kwa Mjomba!