Tuanze safari yetu ya pamoja kutafakari hali na mustakabali wa maisha ya Kijijini Kwetu. Haina maana ya kule nitokako bali hata kwako pia. Yawezekana huna ukakika kama sitafika! Karibu sana
Thursday, April 28, 2011
Ole wenu Mnaoua watu!
Tuesday, April 26, 2011
Hivi tuko wapi vile?
Sunday, April 24, 2011
Leo ni Siku ya Kuzaliwa bi mdogo Maria Fidelia
Leo ni siku ya kuzaliwa bi mdogo Maria Fidelia almaarufu Nkugi.
Ametimiza miaka Mitatu leo….twamuombea maisha mema na baraka tele!
Nichukue fursa hii pia kuwatakia PASAKA Njema ninyi na wapendwa wenu!
Wednesday, April 6, 2011
Ukitaka kwenda Loliondo Jiandae!
Leo nikiwa Mugumu Serengeti nimekuta watu wakiwa wamekaa makundi makundi wakisubiria magari ambayo hayajapewa vibali kwenda samunge Loliondo. Jinsi tu walivoonekana walikuwa wamejichokea hata kabla hawajafika. Pia nimekutana na magari yakielekea Loliondo!
Nikiwa njiani jirani na kijiji cha Kyandege nimekutana na basi la Bedui likitoka Loliondo likishusha mwili wa mmoja wa wagonjwa….ulikuwa umeharibika na kutoa harufu sana.
Maiti ikitolewa kwenye Buti
Wakiuandaa mwili tayari kuuweka kwenye jeneza
Pamoja na haya machungu nilokutana nayo pia nimeshangaa watoto ambao walipaswa kuwa shule wakichunga ng’ombe na kuunza maziwa barabarani!
Taswira…Robben Island!
Boti ya kuwapeleka watalii Kisiwa cha Robben! Ni mwendo wa dakika 30 toka eneo la Waterfront, Cape Town
Nikiwa na Mkuu was Kanisa la Anglikana Tanzania Akofu Mkuu Valentino Mokiwa tukielekea Robben Island
Twakaribia
Selo ya kwanza ya kufikia wafungwa enzi hizo na iliweza kubeba/kukaliwa na watu 60. Dr Kassala akiuliza swali kwa guide ambaye naye alishawahi kufungwa hapo kwa miaka mitano
Menyu kulingana na daraja…hii ni kwa waafrika na wahindi/colored
Mojawapo ya maeneo ya wafungwa kufanyishwa kazi ngumu(quarry). Tundu linaoonekana ndimo walijihifadhi kwa kuepuka jua na kujisaidia…ktk mtindo wa ‘utajiju’.
Hapa ni kwenye chumba cha Mzee Madiba…aliishi humo miaka 18 kabla ya kuhamishiwa kwenye jela nyingine huko Cape Town kwa miaka 9 wakati mazungumzo yanafanyika ambayo yalipelekea yeye kuachiwa huru.
Safari yoyote ile iwe ya ukombozi ni ngumu. Cha muhimu hakuna kukata tamaa.
Maji Ni Dawa!
Kuna baadhi yetu hawapendi kunywa maji…utakuta mtu anamaliza siku kadhaa bila kunywa maji!
Nakusihi, kunywa maji kwa kadiri uwezavyo!
Monday, April 4, 2011
Tunajiandaaje?
Hivi karibuni yametokea matetemeko ya ardhi huko Ujapani yakiambatana na sunami na kusababisha mafuriko na kinu cha nyukilia kuvujisha mionzi….
Mwezi wa pili mwaka huu 2011 nilipata fursa ya kutembelea mtambo wa nyuklia wa kuzalisha umeme huko Cape Town Afrika Kusini. Tulielezwa kuwa wanazalisha umeme zaidi ya 40,000mW na wanatarajia kujenga vinu vingine.
Taswira za ziara ya kutembelea kinu cha nyuklia.
Hapa kwetu huko Bahi, Manyoni, Njombe na Namtumbo kumegunduliwa madini ya Uranium ambayo yanatumika kwenye hivi vinu. Tumejiandaaje kukabiliana na athari zake? Tayari tumeshaona wakubwa wakifurahia uwepo wa madini haya bila kujali athari zake kwa watu kiafya na mazingira.
Kama tunashindwa ktk madini mengine ya dhahabu tutaweza kweli kweye hili?
Friday, April 1, 2011
Tunayo safari Ndefu
Bado najiuliza uongozi hapa kwetu unatafutwa kwa ajili gani. Imekuwa sasa kama kasumba….Maraisi wawili wakihojiwa na waandishi wa habari wa nje wamekiri kuwa hawajui kwa nini Tanzania ni maskini. Sumaye akitoka Harvard naye akadai kuwa kwa miaka 10 alokuwa waziri mkuu hakujua kwa nini tuko maskini….na kwa vile ametoka huko sasa anajua.
Wiki hii Pinda naye kasema hajui.
Tunayo safari ndefu….