Kwa takribani wiki moja na ushei sikuwepo hewani hapa kijiweni. Nilikuwa Cape Town, Afrika Kusini ambako kulikuwa na kusanyiko la wakuu (CEOs) na wafadhili wa makampuni ya madini duniani ambako walikutana kwa siku kadhaa kujadili mambo yanayohusu uwekezaji ktk sekta ya madini na hasa ktk bara la Afrika. Kusanyiko hili hujulikana kama Mining Indaba.
Mwaka jana kusanyiko hili lilikuwa na washiriki 4000 lakini mwaka huu kulikuwa na washiriki zaidi ya 6000 wakati kukiwa na makampuni ya uchimbaji madini zaidi ya 2000 toka kote duniani.
Ili kushiriki na hao wakubwa ilikupasa ulipe Rand 15,000 ama dola za kimarekani 2400. Bei ya ushiriki kwa makampuni pia ni tofauti. Mazungumzo yao 95% ni juu ya namna watakavyopata faida, asilimia 4.6 ni namna wanavosaidia jamii (corporate social responsibility) and asilimia 0.4 ni jinsi uwekezaji wao unavoathiri mazingira na baioanuai! Kwa kifupi walikuwa wanazungumzia “how to capitalize the profits and socialize the costs”!
Serikali yetu iliwakilishwa na Naibu Waziri wa Madini, Kamishna wa Madini na Mkurugenzi wa STAMICO! Serikali yetu ilikuwa na banda lakini halikuwa na taarifa zozote hivo manake ni kuwa wamelipia bure.
Jamani, wakubwa hao wanasema kuwa Ulaya, Marekani na Australia wameweka sheria na sera zinazowabana….. hivyo tumaini pekee ni Afrika ambapo hakuna sheria na sera za kuwabana na hata kama zipo wanaweza kuwabana viongozi wa serikali wakazibadilisha ili kuwaneemesha wao!!
Kaazi kweli kweli!