Monday, October 10, 2011

Oyaa...UDsm msituzingue!

Uongozi unapolewa sifa na waongozwa na hutaka sifa? Bila shaka sivyo....lakini ndo maisha yetu ya sasa.

UDASA sasa wana mpango wa kumtunukia Rais J Kikwete shahada ya udaktari kwa mchango wake wa kupunguza malaria.

Prof. mmoja anauliza: ni nini hii lakini?
Anajibiwa kuwa wameleta vyandalua vya bure kila kaya.
Mmoja anauliza: mbona mimi hivyo vyandalua vya bure havitoshi kwenye kitanda cha watoto achilia mbali cha kwangu?

Anapewa jibu: solution ni wewe kupunguza ukubwa wa kitanda! Ama!!!!

Mmoja amefunguka: acheni kujikomba...kama ni mchango wake kwenye afya wanaostahili kumpa ni Muhimbili ambao kwa kumbukumbu zetu tayari keshapewa. Kwa nini ninyi mumpe nyingine wakati si eneo lenu?


Nabaki na maswali: kujikomba? Ili iweje? Ili mpate consultancy serikalini?


Mmmmmh....maisha bongo bana!

1 comments: