Hapa ni kijiji cha NRONGA kipo Machame juu, Mkoani Kilimanjaro
Maziko yalifanyika jana tarehe 29 mwezi huu...misa na maziko yalikuwa sambamba na mama mwingine ila yeye hakuwa askari (Domina Lema) baada ya shughuli za kuzika kawaida askari 6 na kiongozi wao jumla 7 wakacheza gwaride lao na kufyatua risasri tatu hewani kumuaga mwenzao PC Meshack Urassa ambae kituo chake cha kazi kilikuwa Mbeya na alianza kazi 2009.
Maelezo ya askari wenzake walisema amefikwa na mauti baada ya kuvamiwa na majambazi na kupigwa na kitu kichwani..inahisiwa ni nondo zinazotawala huko Mbeya.
Askari waliwasilisha michango yao kwa wafiwa...askari wenzake marehemu, wa huko Mbeya walichanga milioni moja ikakabidhiwa pale makaburini, pia kulikuwa na michango mingine huko Mbeya zaidi ya milioni 2, baadhi zikatumika kufanyia safari na zikasalia laki 9 na nusu nazo zikakabidhiwa kwa wafiwa........


Nini sababu ya NONDO huku na huko? Mifumo mibovu!
Nini sababu ya NONDO huku na huko? Mifumo mibovu!
0 comments:
Post a Comment