Tuesday, November 23, 2010

Unapokubali kuoa ama kuolewa na picha!

 

index

Jamaa kakamata chake!

Jumamosi na Jumapili kulikuwa na sherehe ya kukata na shoka baada ya binti wa miaka 13 kufunga ndoa na kijana aliyeko Dar akisoma chuo! Binti huyo aliyemaliza darasa la saba mwaka huu anatarajiwa kuingia sekondari mwakani (wakati wa kampeni tulielezwa kuwa watoto wa darasa la saba sasa watakuwa wanaingia moja kwa moja kidato cha kwanza!!).

 

Kwa bahati mbaya yawezekana atakapoitwa kujiunga na shule atakuwa amembeba mtoto mwenzie mu-tumbo mwake!!!!

 

Kioja ni kuwa muoaji hakuwepo ila aliwakilishwa. Nilijiuliza kama MC akisema ‘sasa Bwana na Bi Arusi wanakwenda kujipumzisha itakuwaje?’ Hii inanikumbusha stori ya wapare (akina Mt Simon na Da Koero) kula ugali kwa picha ya samaki!!

Haya ngoja twendelee kuangalia sinema hii.

Thursday, November 18, 2010

Tutarajie miaka 5 ya kisasi?

Labda ni tanzania pekee ambapo yanayosemwa hutendwa kinyume inapokuja kwenye utendaji kisiasa!

Tuliambiwa gesi imepatikana na umeme utapungua bei lakini tunaona umeme ukipanda bei kila siku. Tuliambiwa wawekezaji wakija ajira zitakuwepo kedekede na kwamba uchumi utapanda na maisha yatakuwa bomba sana lakini hali halisi mifukoni mwa watu wa vijijini na hasa walioko maeneo ambako kuna wawekezaji hali ni hoi kuliko tulivoaminishwa, n.k, n.k.!

 

Sasa uchaguzi umeisha na chama chetu kimeshinda kwa ‘kishindo’ huku vyama vya ‘upinzani’ vikichukua majimbo muhimu kwa ‘chama chetu’. Hapo ndio ngoma inapoanzia kwa kuwa katika uzoefu mdogo wa tangu mfumo wa vyama vingi uanze mahali ambapo kuna kiongozi wa upinzani maendeleo yamekuwa hayapo kwa makusudi ya kuwatia watu adabu.

 

Hapa Musoma kwa mfano, CHADEMA imepata uwezo wa kuunda baraza la madiwani na pia wamepata mbunge…minong’ono iliyopo ni kuwa ‘tutaona watafika wa’! Unaweza kukuta kwa miaka mitano ijayo eneo kama hili na watu wake wakinyimwa fursa za maendeleo kwa kisingizio cha kijinga cha kuwakomoa ati kwa kuwa walichagua ‘upinzani’. Na ukiangalia ususwaji huo huwa haubagui wa chama tawala ama upinzani.

 

Unaweza kukuta mikoa takribani 10 ambayo imepigia kura upinzani mwaka huu ikasuswa na zile ahadi walizopewa wakati wa kampeni zikayeyukia hewani. Na unaweza kukuta wale wabonge walomkataa waziri mkubwa wakiandamwa na mkubwa huyo hata kama alisema katika hotuba yake kuwa hatawashughulikia!

Kitendawili kitateguliwa na wao wenyewe!

Monday, November 8, 2010

Taswira za ushangiliaji ushindi

Uchaguzi umeisha lakini kwa hapa Musoma, ni uchaguzi utakaokumbukwa sana kwa kuwa na matukio kabla na baada ya uchaguzi. Inasemekana katika jimbo hili la Musoma Mjini ni NADRA kwa mbunge kutawala vipindi viwili! Kwa mfano Ibrahim Marwa (ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Same) alikuwa mbunge kwa miaka 5 tu kabla ya kung’olewa na mbunge aliyemaliza muda wake ambaye ameng’olewa na Vincent Nyerere wa CHADEMA. Sina hakika kama huyu atadumu vipindi viwili lakini wananchi wataamua hapo baadaye!!!

 

CHADEMA ilinyakua jimbo na udhibiti wa halmashauri ya Manispaa kwa kupata Madiwani 8, CUF 2 na CCM 3 ambapo mmojawapo wa CCM amekataa kutia saini kuwa AMESHINDA!!!!! Jamani fursa inakuja weye waikataa?….lol! NItalijadili hilo baadaye panapo majaaliwa!

 

Pata taswira za ushangiliaji ushindi siku ya tarehe moja mwezi Novemba kwa kuwa mbunge huyu mteule alikuwa wa kwanza kutangazwa kwa nchi nzima…usiniulize kwa nini labda ntakueleza tutakapoonana kwenye kahawa….lol!

01112010023

Mamia ya washabiki wakielekea nyumbani kwa mbunge Mteule kujiunga na wenzao kushangilia.

01112010024Mashabiki wakishangilia na kuufanya mji wa Musoma kuzizima kwa muda

01112010027 

   01112010025

Palikuwa hapatoshi!

01112010028  

  01112010029

Nadhani kwa mara ya kwanza (kwani sijawahi kuona ama kusikia live) staili mpya ya ushangiliaji ikaonekana hapa mjini! Nyuma ya gari na picha inayofuata wakaonekana mashabiki wakiwa na jeneza la kiislam lilotengenezwa kwa neti ya kuzuia mbu na likiwa na picha ya mgombea wa CCM!!!! Hawakuishia hapo pikipiki moja almaarufu ‘bodaboda’ ilionekana ikiwa imebeba jeneza litumikalo na wakristo huku wakiimba kuwa wanakwenda kumzika mgombea aloshindwa!

 

Binafsi sikufurahia jambo hilo lakini ni historia ya kukumbukwa mwaka huu!!!!