Aina za kulala!
Kaka Ngw’anambiti, pole na majukumu! Mimi ni msomaji wako katika kijiji chako ambacho sijui nani alikuchagua kuwa mwenyekiti wake! Nimekuandikia kutaka mchango wako wa mawazo. Unaweza kubandika hapo kwenye ubaraza wako ili wengine wajifunze kupitia suala linalonikabili. Naitwa mama John (si jina halisi) na niko Dar.
Mimi ni mama wa watoto watatu. Mimi na mume wangu tulioana wakati tukiwa wabichi kabisa kutoka chuoni na sasa tunakaribia miaka 12 tangu tuoane. Siku za hivi karibuni nimekumbwa na tatizo moja. Niligundua kuwa mume wangu hana hamu nami kabisa na tunapopata nafasi ya kujamiiana huwa anapiga ‘bao moja tu’ na kuchoka kitu ambacho si kawaida yake. Nilimuuliza lakini hakutaka kuwa muwazi kwangu japo alisingizia kuwa ni kuchoka tu na mihangaiko ya mchana.
Majuzi tulipata mgeni nyumbani kwetu…mdogo wangu wa kike asomaye chuo kikuu kimoja hapa nchini. Ilikuwa akae nasi mpaka watakapofungua chuo mwezi wa 11 baada ya kunyimwa fursa ya kuwa chuoni mwezi wa 10 kama ratiba inavyoonyesha katika prospectus zao.
Alipofika, baada ya muda akanilalamikia kuwa shemejie anamtaka kimapenzi na hivyo anataka kuondoka hapo nyumbani aende kijijini kwani hataki kuleta usumbufu katika familia yangu. Baada ya kufikiri tulikaa na kuzungumza na mdogo wangu na tukaamua kuwa ni lazima tufanye kitu ili kuzuia ubaradhuli wa namna hii usirejee tena kwake na kwa wengine.
Tulikubaliana kuwa mdogo wangu amkubalie na wapange kukutana usiku baada ya mimi kulala. Kwa kuwa muda mwingi huwa anarejea nyumbani usiku na kwa kuwa chumba cha wageni alalacho mdogo wangu kiko karibu na sebule atamgongea dirishani kasha atamfungulia. Tulikubaliana kuwa siku ya siku mimi ndie nitalala kwenye chumba hicho nay eye atakwenda kulala chumba cha watoto na kazi ya kufungua mlango nitaifanya mimi.
Alimweleza kuwa ‘ombi lake limekubaliwa’ na wakapanga kuwa wataonana jioni na kuwa agonge dirisha. Baada ya kula jioni mdogo wangu alikwenda kulala chumba cha watoto na mimi nikazima taa ya sebuleni kasha kulala chumba cha wageni. Mume wangu alikuja akagonga dirisha na nikaenda kumfungulia mlango. Kwa sababu ya giza hakuweza kunitambua na akavua viatu ‘visipige kelele vikaniamsha’ nakujitoma chumba cha wageni kimyakimya. Alinivamia na kuanza shughuli.
Naomba niseme kuwa alipiga bao 4 non-stop huku akinisifia (akidhani kuwa ni mdogo wangu) kuwa nayajua majambo. Kisha akatoa wallet (gizani) na kuipa pesa laki moja!!! Kabla hajaondoka nilimwambia nikimnong’oneza kuwa angoje nikamfungulie. Nilikwenda nikawasha taa na alipatwa na mshangao na mshtuko kuniona ni mimi!!!!
Nilimwambia, ‘baba John, kumbe ndivyo ulivyo?’ Sikuendelea ila kulia kwa uchungu na aliniomba msamaha kwa kitendo kile kwani nilimweleza A-Z kuhusu jinsi alivyofanya.
Najiuliza, kwa nini mimi nilikuwa napewa nusu dose na kwa ‘mdogo’ wangu ikapatikana full dose? Je wanaume wote mko hivyo? Naomba msaada wa mawazo…nifanyeje? Je hatanitenda tena?
Haya wadau, naomba msaada wenu wa mawazo…Kaka Kaluse na Kamala uwanja ni wenyu kwani hili nadhani ni suala la kiutambuzi pia japo linajumuisha saikolojia pia!