
Kutokana na kuamini kwangu juu ya utakatifu wa ndoa na umuhimu wa kuitenga na kila kitakachoivuruga au kuichafua;
Nakutumia nasaha hizi kutoka moyoni, juu ya namna tutakavyoishi katika kipindi cha mashindano ya mpira ya Kombe la Dunia; Ili tutoke na madhara machache kadri inavyowezekana...
Na hizi zifuatazo ndiyo nasaha za mumeo mpendwa:
1. 1: Katika kipindi cha kuanzia tarehe 11 Juni mpaka tarehe 11 Julai njia pekee itakayokuwezesha kufungua mazungumzo kati yetu ni kuwa ufuatilie magazeti ya michezo na habari za kombe la dunia. Na ni kwa njia hii tu itaniyumkinia kushiriki nawe katika mazungumzo na majadiliano... Na utakapoleta maongezi mengine yoyote nje ya mada ya Kombe la dunia basi nitalazimika (nasikitika kusema) kutokujibu, na hili ni jambo ambalo litakalo kuudhi.
2. Na katika kipindi hiki cha kombe la dunia TV itakuwa ni mali yangu kwa muda wote. Na nikikuona unaiangalia Remote Control, basi utapoteza moja ya macho yako mazuri.
3. Kama utataka kupita mbele ya TV wakati wa mechi, au kabla yake au baada yake, mimi sitokuzuia, endapo tu unapita huku unatambaa kama komadoo wa jeshi wakati wa vita kuu ya dunia.
4. Wakati wa mechi ni lazima utambue kuwa mimi sisikii wala sioni na wala siongei, isipokuwa kama nitahitaji chakula au kinywaji, na sitokubali kusikia maneno kama vile; jibu simu, au katuletee hiki kutoka dukani au kafungue mlango...
5. Kama utatekeleza hayo hapo juu basi nitakuruhusu kuangalia TV kuanzia saa 8 usiku mpaka saa 12 asubuhi kwani hakuna kipindi kitakacho nihusu...
6. Nakuomba, kasha nakuomba na tena ninakuomba sana mke wangu, tafadhi usiniambie maneno yako ya kunipoza kama vile eti huo ni mchezo tu, au eti watashinda mechi nyingine, kama utaniona nimehuzunika kwa sababu timu ninayoishabikia katika kombe la dunia imepoteza mchezo, kwa sababu hayo maneno yako hayatonisaidia bali huenda yataniongezea hasira na uchungu na yanaweza kusababisha mmoja wetu kulazwa hospitali na mwingine kufungwa jela...
7. Sina kikwazo kama utakuja kuangalia mechi pamoja na mimi, na nitakuruhusu kuongea wakati wa mapumziko endapo tu matokeo ya mchezo yanaelekea kuwa mazuri kwa timu yangu. Nakuomba upigie mstari swala la matokeo kuwa mazuri.
8. Marudio ya magoli katika TV ni muhimu sana kwangu na sina tabu hata kama nitaliangalia goli moja mara 100, usishangae.
9. Katika muhtasari wa kila siku wakombe la dunia sitaki kusikia unasema mechi umeshaiona, kwa nini unaangalia tena muhtasari. Jibu langu litakuwa: angalia namba 1 na 2 za barua hii.
10. Baada ya fainali za kombe la dunia nakuomba usiseme Alhamdulillah kwamba kombe la dunia limekwisha na halitokuja tena mpaka baada ya miaka mine, kwa sababu maneno kama hayo hayana nafasi katika kichwa changu. Nakuomba usisahau kuwa kuna kombe la Euro, Euoropean Championship, Europa, English Premier League, FA Cup, Ligi kuu ya Spain, Italy, n.k. Hivyo naweza kuamua kwa wepesi kabisa kulipizia kile nilichokikosa katika kombe la dunia
Nakushukuru mke wangu kwa kunisikiliza na kukubali kushirikiana nami katika hili.
Mumeo mpendwa ...
Chanzo: Mtandao wa upashanaji habari wa www.thefoundation-tz.org