Friday, April 30, 2010

Kila la Kheri siku ya wafanyakazi-MEI MOSI!


Pamoja na salamu za Mei Mosi hapo kesho, nawatakia wikiendi njema na kibonzo hiki!

Wednesday, April 28, 2010

Unapokaribishwa na mbu inakuwaje?

Inapendeza wakati mwingine unapokaribishwa nyumbani na watu kwa bashasha :-)

Lakini inashangaza zaidi pale unapokaribishwa na mbu na wakakuweka kiti moto :-(
Mtakatifu Simon amekaribishwa kwa bashasha za aina yake mji kasoro bahri (Morogoro) na mbu wa KILAKALA na kumpiga stop kwa muda a.k.a kumuwekea spid gavana asitembee.

Kwa niaba ya wadau nampa pole na kumtakia afya njema.

Get well soon kamarade!!!!

Wewe tu

Pendo likishamdondokea mtu haliangalii chochote kile


Mpenzi wangu sikia,
Maneno ninayokwambia,
Kwamba nakupenda,
Wewe.
Nitakuja hadi kwenu,
Niwaone wazazi wako,
Niwaambie nakupenda,
Wewe.

Niahidi utanipenda,
Siku zote maishani,
Kwa kuwa nakupenda,
Wewe.
Kwangu hakuna mwingine,
Nitayempenda zaidi,
Niamini nakupenda,
Wewe.

Najisikia fahari,
Ninapopendana nawe,
Nitazidi kukupenda,
Wewe.
Sogea karibu nami,
Nilipate pendo lako,
Nizidishe kukupenda,
Wewe.

Shairi hili limetoka hapa nami nimelipenda kwa hakika.

Tuesday, April 27, 2010

Kwako Mwanamke wa Shoka, Mija! Hongera!

Leo ni siku yako tukufu kwa kuwa unaadhimisha ile tarehe ulofika duniani
Nakutakia kila la kheri katika maisha yako.
Hepi besdei!!

Friday, April 23, 2010

Hongera kwa BirthDate Yako


Anaitwa NKUGI na kesho tarehe 24 atatimiza miaka 2 kamili. Sina hakika na siku alozaliwa lakini nina hakika na tarehe alozaliwa ndo ya kesho. Nawahi kubandika kwa kuwa tumetangaziwa kuwa hatutakuwa na umeme/stima kesho kuanzia asubuhi.

Tofauti na wengine wenye maombi mahsusi kama wa Matondo yeye ni furaha kwa kitu chochote atakachoona
mbele yake.


Kwao mara nyingi wanamuita jina la kati yaani Fidelia kwa kuwa jina alopewa ni Maria Fidelia Nkugi.

Huyo ni yule anayeonekana akiwa na mwenye kijiwe akiwa na uwoga kama anavoonekana pale kwa Matondo wakati akiwa na Kamala anaonekana kudeka....lol!

Napenda kumpongeza kwa kutimiza miaka 2.

Je wewe ni Mbu?

Jana nilihudhuria maziko ya Mama Mkwe wa mdogo wangu alofariki kwa tatizo la INI akiwa na miaka 84 huko kijijini kwetu.

Ni maziko ambayo hayakuwa na vikorombwezo kibao kama mapicha ya video nk. Mashada nayo yalikuwa ya kawaida ambayo yalitokana na miti na nyasi zilizokatwa na kukunjwa kiaina.

Maziko yaliendeshwa na Padre ambaye ni paroko wa kanisa-mahalia na nimevutiwa sana na sehemu ya mahubiri yake kwa jamii ya kileo.

Injili iloyotwangwa ilikuwa ile ya wanawali werevu walokuwa na mafuta wakati wa kumlaki bwana arusi na wapumbavu ambao hawakuwa na mafuta. Pamoja na kauli za kawaida za vitisho vya kawaida za viongozi wa dini hasa ktk nyakati kama hizo katika homilia zao, jambo moja lilinigusa.

MBU: Paroko alisema sasa hivi watu tunaishi kama MBU katika jamii. Mbu tabia yake ni kueneza ugonjwa wa malaria. Kwa usiku mmoja anaweza kueleza kwa watu lukuki, watoto, wamama, wababa, wazee nk.

Jamii yetu nayo imekuwa hivo hivo. Maisha tunayoishi yamekuwa kama ya mbu ya kueneza magonjwa. Mahusiano kati ya mtu na mtu yako hovyo. Mtu anaweza kugombanisha mtaa ama ofisi nzima kwa fitna na majungu. Na inakwenda mbali na hapo: mtu sasa anajifitinisha yeye mwenyewe katika nafsi yake!

Swali: Katika mazingira yako, wewe ni mbu?

1: Mtu mmojammoja: je unatimiza wajibu wako ktk familia, pahala pa kazi, jamii nk?

2. Chama cha siasa, wewe ni mbu? Unaeneza siasa za chuki na mafarakano katika jamii badala ya upendo amani na mapatano? Je unahubiri uwazi, uwajibikaji, nk wakati wewe unafanya tofauti kwa kukumbatia ufisadi?

Na tuapoelekea muda huu wa UCHAGUZI tutashuhudia MBU wengi sana.
Wakati utatuambia kama sisi ni mbu ama la!

Thursday, April 22, 2010

Utaalamu wetu wa asili uko wapi?



Kuna mdau kaleta ishu hapa ambayo haiwezi kupita bila kujadiliwa. Hoja hiyo ilokuwa na kichwa cha habari
Mbegu walete wao, kulima nilime mimi, tena kwa sululu inafikirisha sana hasa juu ya upatikanaji wa mbegu!


Nina shida na makampuni yanayouza mbegu. Makampuni hayo kama Mosanto nk yote toka nchi za mabwanyenye wa dunia hii. Sasa tumefikia hatua ambapo mbegu hizi zinakuwa zimebadilishwa vinasaba (genetically modified).


Wadau mbalimbali duniani wanapinga hoja ya watu kupewa bure ama hata kwa kununua kwa kuwa si endelevu.Hizi ni mbegu unazoweza kuzipanda kwa msimu mmoja tu na wanafanya hivi ili kutukamua hata vile vipesa viduchu tunavomenyeka kuvitafuta.


Mbali na hayo wafanyabiashara hawa hawajali kabisa mambo muhimu ya kuzingatia.


1. Hawajali juu ya mbegu zenye kuhimili mabadiliko ya hali ya tabia-nchi (climatic Change) na ukame


2. Hawajali kabisa ladha ya hicho kinachozalishwa. Mtakubaliana nami kuwa zamani mahindi yetu yalikuwa na ladha tamu tofauti na ladha ya mahindi haya tulionayo siku hizi. Nakumbuka enzi zile miaka ya 70 ukipita nyumba ya jirani walipopika ugali wa mahindi utajua tu kutokana na harufu na pia tulikuwa tunakula ugali bila hata mboga kutokana na utamu/ladha yake tamu. Wenyewe tuliita 'reghureghu'.


3. Hawajali kabisa uendelevu wa mtu maskini na pia uwezo wa wananchi wetu wa kuchagua na kutumia mbegu zetu wenyewe. Wanasisitiza kuwa zetu hazifai. Zamani (na jamii chache sasa zimebaki na utaalamu huu) tulikuwa tukishavuna tunachagua mbegu na kuziingika juu ya paa juu ya meko ili kuzuia wadudu wanaobungua mbegu hizo. Na msimu ukifika anachukua mbegu hapo alipoziweka na kuzipeleka shambani. Kwa wale wasiokuwa na mbegu bora iliruhusiwa kwa jamii kubadilishana mbegu kulingana na mahitaji.


Sasa hali si hivo...sasa tunatakiwa kununua kila mwaka kwa kuwa hizi za madukani huwezi kulima misimu miwili mfululizo.


4. Hawaangalii aina ya udongo tulio nao. Na matokeo yake ni kwamba kwa kuwa zinatumia madawa/mbolea za viwandani kwa kiwango kikubwa.


Hapa ndo kuna changamoto kubwa kwa KILIMO KWANZA.


Kwamba kila mwaka mtu wa kijijini auze mbuzi wake ili anunue mbegu na pia mbolea.


Huu ni UTUMWA MPYA!

Monday, April 19, 2010

Unapokosa Uazime?


Wazee wa Wilaya ya Geita wamefanya mazungumzo na wazee wa Kigoma Kaskazini ili kupata ridhaa yao ili kumruhusu Mh. Zitto Kabwe kuwania ubunge mwaka huu huko Geita.

Wamesema " kwa mujibu wa mila na desturi za Kisukuma, sio kosa wala aibu kuazima dume kutoka kwa jirani ikibainika kuwa linafaa ".

Dume hilo linaitwa NZAGAMBA kwa kisukuma....lol

Je kama trend ndo hii ya kuazima, hatutafika wakati tukaazima RAIS nyumba ya jirani? :-(

Friday, April 16, 2010

Si rahisi kueleweka!

Ndiyo! Ni vigumu kuwa elewa wanasiasa!

Wakati wanakiri kuwa tu maskini wakati huohuo wanakiri kuwa tu matajiri wa rasilimali!

Inashangaza basi kwa Mkuu wetu wa nji kupita na kapu akiomba ilhali tuna rasilimali lukuki!

Wakati akifanya hivyo huko ughaibuni serikali yake inakataa kupeleka rasilimali kwa wananchi pamoja na ushauri wooote wa wataalamu na wananchi.

Hii ni serikali ambayo tumekuwa tukiambiwa kuwa inasikiliza watu wake.

Lakini usikilizaji wake inaonekana ni wa kuwasikiliza zaidi wawekezaji na si wananchi waliowaweka madarakani. Ndiyo sababu tunasikia sasa vilio kila sehemu ya nchi.


Wakubwa wanasikiliza zaidi wenye pesa zaidi ya watu wao. Halafu wanaenda kuomba huko kwa hao wanaovuna rasilimali zetu kwa bei ya chee tu.

Hebu burudika na wimbo huu wa Mr Politician wa Nakaaya Sumari ili kutuliza machungu kidogo au vipi?



Au msikilize huyu mwanamziki aitwaye Kala Jeremiah akimshirikisha Nakaaya Sumari na wimbo wake wa Wimbo wa Taifa

Thursday, April 15, 2010

Karne ya 21 na Uchawi!

Kitambaa cha 'Tambiko'

Leo asubuhi saa 1.30 wakati naelekea ofisini nikiwa eneo la Bweri Bukoba Kata ya Bweri Manispaa ya Musoma nilikutana na kituko cha mwaka. Nasema kituko cha mwaka kwa kuwa nilikuwa labda niko nyuma ya wakati kwa kudhani kuwa vitu kama hivo vimekwisha.

Nilikutana na kitambaa cheupe kama kinavoonekana katika picha kikiwa na pesa sh 200 (2) sh 100(4) na sh 20 (1) zinazofanya jumla iwe sh za kitanzania 820.Watu wote walopita eneo hilo walionekana kushangaa na kupigwa na taharuki na hakuna aliyethubutu kuzichukua pesa hizo! Hata niliposhuka katika 'bodaboda' langu ili kuchukua picha hizi kwa kutumia simu yangu watu walinishangaa wakiwa na sura za wasiwasi!

Swali laja:

. Bado katika karne ya 21 kuna watu wanaamini kupata kila kitu kwa njia ya uchawi?

. Ni lini watu watakapoamini kuwa ni katika kufanya kazi kwa bidii tu ndipo kile tunachkihitaji kitakapotimia?



. Je yawezekana tunapoelekea uchaguzi mkuu tukaona mengi zaidi ya hayo?

Hebu tujikumbushe kidogo hapa burudani ya MZEE WA BUSARA na Juma Nature:


Ama tusikie vitimbi vya uchaguzi. Hapa Prof. J., Mc Babu Ayoub na Juma Nature wanawakilisha.

Tuesday, April 13, 2010

Ni kwa masilahi ya wananchi ama ni kwa masilahi ya chama?


  • Watumishi zaidi ya 90 wa hospitali ya Mwananyamala wameondolewa hapo kwa maelezo kuwa wanahamishiwa hospitali zingine ili kubadilisha mitizamo :-(
  • Habari zingine zanena kuwa hatua hiyo imechukuliwa kufuatia ziara ya Mkuu wa Nji alipotembelea hapo katika ziara ya KUIMARISHA CHAMA na kutoa maagizo kuwa kufanyike marekebisho ili kuweka mambo sawa!

MASWALI KADHAA!
  • Je ni mpaka mkuu wa nji atembelee sehemu hata kama kuna uozo ndipo maamuzi yachukuliwe?
  • Je ni kwa maslahi ya chama tu ndipo hali hubadilishwa?
  • Kwa nini wananchi wakipiga kelele kuelezea madhila wanayokumbana nayo watawala wanaziba masikio mpaka kiongozi wa chama akisema mambo yanarekebishwa?
  • Ni lini tutaenda 'beyond CHAMA' na kushughulikia masilahi ya wananchi zaidi?
  • Je kwa mtindo huu maslahi ya wananchi yanaonekana kuwa na mashiko mwaka wa tano baada ya uchaguzi?

Friday, April 2, 2010

Ajali zingine twazisababisha siye wenyewe!

Barabara zetu zina ubora unaotakiwa? Bidhaa hazina ubora, vipi kuhusu watengenezaji?


Mara kwa mara tumesikia juu ya suala la ubora wa vitu vitokavyo Uchina. Kwa sasa soko la bidhaa za kichina limetamalaki hapa Bongo na kwingineko barani kwetu.

Kwa bahati mbaya twaambiwa kuwa baadhi ya vitu viletwavyo yawezekana havina ubora unaotakiwa. Ukiangalia hapa kwa Da Yasinta ama Basilutasoma na kuona madhara ama utamu utokanayo na vitu va Kichina.

Lakini Ze Comedy enzi hizo pia waliwahi kuzungumzia juu ya uduni wa vitu vya kichina. Sasa hali hiyo iko pia katika nyanja zingine.

Kila kukicha biashara inayofanywa na wachina inakua kuanzia umachinga mpaka ujenzi wa barabara. Nakumbuka nilibahatika kuwaona wakijenga kipande cha pili cha barabara ya Mwanza-Nzega ambacho kilikuwa kinaanzia njiapanda ya kuelekea Misasi iliyoko wilaya ya Misungwi jirani kabisa na kijiji ambacho kwa sasa ni machimbo ya kinachosemekana kuwa ni almasi cha Mabuki.

Kuanzia hapo mpaka Hungumalwa kipande hicho ni kibovu tangu kilipojengwa miaka ya Tisini. Nakumbuka kampuni hiyo ya kichina wakati inakuja kujenga waliisifia sana na kuponda ile ya Zakhem (iliyokuwa na kambi yake pale Mkolani-Mwanza) iliyokuwa inajenga kutoka Mwanza hadi Mto Magogo kwa kuwa ati ile ya kiarabu ilipewa tenda kwa upendeleo wa kujuana na Mkulu wa nji wa wakati huo. Hata wasimamizi wa mradi (Becca Worley International na wenzao wa hapa nchini Design Partnership) walikuwa wanaifagilia sana hii ya kichina. Cha ajabu ilifanya vibaya.

Pengine utasema huyu jamaa sasa anawaharibia hawa ndugu zetu. Kuna ushahidi mwingine wa barabara kuu ya Shinyanga-Singida ambapo kipande cha Shelui kwenda mpaka Misigisi kupitia kwenye ule mlima wenye maajabu wa Sekenke kiko hoi ilhali imezinduliwa miaka ya karibuni.

Kwa jinsi hali hii inavyokuwa nina wasiwasi kuwa hata kile kipande cha Singida Manyoni ambacho nacho kinajengwa na wachina kikawa bomu.

Ndiyo kusema hatuna wataalamu wa kusimamia na kuona kuwa mambo yanakwenda shwari ama kuna sababu nyingine? Nakumbuka kuna kisa cha baadhi ya viongozi wa serikali kumlaumu Padre Thomas Bilingi wa Jimbo Katoliki la Geita ati kwa kuwa kila alipopita katika mojawapo ya barabara zinazopita parokiani mwake ilokuwa ikijengwa alionekana akichukua 'futi' kupima upana na kina cha barabara na kisha kutoa mahubiri kanisani jumapili ilofuata kuwa bababara hiyo ni mbovu kwa kuwa haikujengwa kwa viwango vinavotakiwa!

Kwa kiasi fulani naungana na Pd Bilingi kwa kuwa kama mtu nilosomea masuala hayo ya barabara na nyumba kipindi fulani huwa nikipita katika baadhi ya barabara zetu huwa najiuliza kama kweli viongozi wetu wanapokwenda kuzindua barabara zetu huwa na taarifa kama tushaibiwa ama la?

Ngoja nikatafute pahala yalipo MACHICHA nipooze kiu!