

Nilifukiwa nusu mwili ili
kuwawezesha wazazi kulima
kwa raha bila karaha!
Nakumbuka simulizi za baba na mama yangu wa kule Ryakahenge enzi hizo nimezaliwa hakukuwa na 'Housegirls’! Wananisimulia kuwa wakati wakiwa wanakwenda shambani ilikuwa inawapasa kuchimba shimo na kunizika nusu kama njemba hapo juu kwenye picha.
Hapo ningelia weeeee mpaka basi. Ningejinyamazia na kula mchanga kama sina akili njema. Thanks God enzi hizo LABDA magonjwa hayakuwapo kwa kuwa tulikuwa hata twatembea uchi bila nguo na hakuna cha NYUMONIA wala nini. Siku hizi mtoto atembee kifua wazi tu utasikilizia muziki wake…lol! Sijui ndo utawazi huo ama?
Sasa enzi hizi katika malezi ya watoto kuna kitu kinatisha sana. Wengi wetu tumeajiri wasichana wa kazi watusaidie kulea wakati tumejielekeza katika kazi za kujitafutia riziki.
Matokeo yake tumesikia madhara kibao yatokanayo na malezi kwa watoto ama hata vifo kwa watoto kwa sababu ya kutopata matunzo muhimu kama chakula, usafi na kadhalika.
Tumesikia pia kuwa wasaidizi hawa wa ndani aidha wakiwaleta watu (vijana wa kiume) nyumbani ama akimfungia mtoto/watoto na kutokomea kwenda misele na hivo kuhatarisha usalama wa watoto na mali.
Swali: Katika nchi nyingine baba na mama wanapata likizo ya uzazi tofauti na huku kwetu.
Je ni njia ipi bora ya kumpa matunzo mtoto mdogo kabla hajajitegemea ikitiliwa maanani kuwa baba na mama wana majukumu mengi ya kikazi?

