
Shule zetu na maandalizi ya kizazi kipya!!!
Taifa la kesho?
Kila siku tumekuwa tukisikia juu ya serikali yetu kutilia mkazo juu ya elimu ya msingi na kadhalika. Hata hivyo sina hakika kama hili lina kuwa na maana kwa kuwa ukiliangalia kwa undani utaona kuwa ni kama tunacheza mchezo wa kuigiza!
Kwa mujibu wa waraka wa elimu (sijui niiite sera) wa 1995 serikali yetu iliazimia kuhakikisha kuwa elimu ya awali inatiliwa mkazo katika kila jambo.

Leo hii timu yetu ya mpira ikifungwa ama Yanga na Simba zikishindwa utasikia wakubwa wanasema 'kuna haja ya kuhakikisha kuwa vipaji vinaibuliwa kuanzia utotoni'!
Picha hii hapo kulia ni shule ya awali a.k.a chekechea ambayo niliikuta kijiji cha Loswaki kilichoko kata ya Terat wilaya ya Simanjiro nkiwa huko kishughuli. Hii ni shule inayotegemewa kuibua vipaji na kutoa viongozi na wataalam wa kizazi kijacho!
Nasema hivo kwa kuwa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Asasi ya MWDA ya Mwanza huko wilayani Kwimba ulionesha kuwa wakati shule za msingi kuanzia madarasa ya kwanza mpaka saba wanapewa ruzuku, aidha hakuna madarasa ya awali (kama inavoelekezwa ktk sera) ama kama yapo hayapewi ruzuku kama inavotakiwa kwa mujibu wa sera zilizopo.
Cha kushangaza ni kuwa viongozi wetu ni kama hawaelewi kitu wanachokiweka ktk makaratasi iwe ni ktk sera ama sheria zinazotungwa pale mjengoni au hawataki kuelewa kwa makusudi.
Kama ni kwa makusudi tuna haja ya kuwa na watu kama hawa ambao wengine wakiwa ni wataalamu waliobobea katika taaluma zao?
Je tumefikia hatua ya kuamini kuwa hakuna lolote tunalolipanga ambalo litakamilika ati kwa kuwa walioko Tanzania (Dar) hawataki, hawaelewi ama hawawezi kuchukua hatua katika kuhakikisha kuwa elimu yetu inakuwa ya maana kama kule ambako wao hupeleka wana wao kusoma?
Je ndiyo sababu ya kuanza kudharau taaluma ya ualimu kiasi cha kuanzisha program za ualimu za ' voda fasta' ambapo vijana wetu (wenye msingi mbovu wa elimu) wanaingizwa ktk program ya kuwa walimu kwa muda wa miezi 6 tu!
Nadhani haitoishia hapo kwa kuwa sekta itakayofuata yaweza kuwa AFYA ambapo madaktari bingwa wa upasuaji wakwenda mafunzoni kwa muda mfupi! Na ikitokea hivo basi TUTAOMBA kwamba watu wa kwanza watakaofanyiwa upasuaji wawe wale wanaopata matibabu yao nje ya nchi!!!!!
TAFAKARI!
